Matatizo ya waislam hayakuanza leo wala jana
Katika historia uislam uliletwa hasa huku afrika na kuenezwa na waarabu
Pia iliaminika kuwa ulikuwa na nguvu sana kuliko dini nyingine lakini kwa ukweli ni kwamba waarabu walikuwa wafanya biashara wazuri na walikuja na elimu lakini ilikuwa na ni elimu ya dini tu
Baadae ndipo walipokuja wamisionari na dini yao ambayo ndio dini ya kristo
Ujio huu wa wamisionari ulikuja na dini, utawala na elimu ya zaidi
Swala ambalo lilifanikisha kuwamiliki waarabu walikuwa wakisambaza dini ya kiislamu
Hii ilitokana na ukweli kwamba wamisionari hao ndio waliokuwa watawala hivyo kuwa na nguvu sana na kuweza kuzima baadhi ya dola za kisilim
Kutoikea enzi za ukoloni ukristo popote duniani umekuwa ukipata misaada ya kifedha na kimawazo kutoka katika mataifa mbalimbali ili kuimarisha utawala wao
Kwa kuwa kipindi chote hicho wakristo walikuwa ndio watawala hata misingi ya elimu waliishikilia wao hivyo ndio waliokuwa na dhamana ya nani apate elimu na nani asipate
Hivyo utaratibu ulikuwa kwamba usiekuwa mkiristo ukitaka elimu basi uwe mkristo mbali na hivyo elimu hupati
Mbinu hii iliwarudisha sana walikuwa tofauti na wakrito na himaya za wakristo zilipata nguvu sana hadi leo
Katika kuimarisha dini ya wamisionari walitumia sana propaganda katika kupata wadau wengi kutokana na nguvu ya neno propaganda yenyewe ilivyo
Propaganda hizi zilitumika katika kuwatia watu woga hasa katika dini ya upande wa pili na kwa wengi walio amini waliaanza kuona uislam kama dini ya shetani,dini ya watu wasiokuwa na elimu na hata kuiona kuwa dini ya kigaidi
Hali hii imeendelea hadi leo ndio maana utakuta waislam kila wanachotaka kukipata kina kuwa kwao ni shida tupu
Mataifa makubwa yanautambua uislam kuwa ukipewa nguvu basi huenda wakakumbuka shida waliopata hivyo hivyo wakalipiza
Haya hanaasababisha Taasisi nyingi sana za kiislam kuvunjika au kutoendela kwani misaada yote ikitolewa na waislam inaitwa ya kigaidi
Waislam wallitaka kujiunga na NIC ilikuwa shida makinisa yakisimamia kidete sasa waislam wanataka kuanzisha mahakama ya kadhi ambayo ki msingi hii ni kwa ajili ya waislam ili kutafuta haki zao za kiislam lakini hata wasiokuwa waislam wana kataa kwa nguvu mi nafkiri kuwa hapa kuna tatizo
Hivi wewe ungepata nafasi ya kutoa maoni yako kuhusu hili ungesemaje?
Monday, July 13, 2009
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment