Monday, July 13, 2009

mahindi ya kuchoma huleta hasara kubwa zaidi ya faida

mahindi ya kuchoma huleta hasara kubwa zaidi ya faida

Na Bashir Salum

Katikamaisha ya watu wa mjini hasa maeneo ya pwani kama mikoa ya pwani,dare s salaam na hata mkoa wa morogoro kwa wale wasiokuwa wakulima au wale wanaopita mji miji hiyo kama watembeaji huweza kutashangazwa na majira ya mwaka katika maeneo hayo


Wapo watu waishio katika maeneo haya ambao hata kufahamu kuwa vuli au maskaa yanaanza lini au yanakwisha lini kwao ni mtihani kabisa lakini hii inatokna na ukweli kwamaba hata zile dalili za upatikanaji wa vitu fulani kwa kipindi fulani humfanya mtu kutambua misimu ya mwaka

Mfano kule kijijini kwangu huwa hata mtoto wa darasa la tatu anaweza kutofautisha vipindi kutokana na kufahamufika kwamba bidhaa kama mahindi maharage vina msimu wake hivy kuelewa fika misimu hiyo


Katika mikoa tulioitaja utakuta bidhaa ya mahindi ya kuchoma inapatikana katika kipindi chote cha mwaka mzima wakati mikoa kama Dar es salam hakuna wakulima wa mahindi

Ukiangalia kwa sasa biashara ya mahindi ya kuchoma imeenea kila kona huwezi kupiupita mji fulani bila kuwaona wawili watatu waaendesha biashara zao

Mimi binafsi siwachuukii wafanya biashara wa mahindi ya kuchoma ambao kwa hapa mjini utakuta ni wengi sana na wanaendesha maisha yao kutokana na biashara hiyo

Lakini! Tufikirie yahaya mahindi yanatoka wapi! Na yanalimwa na nani? Hivi mkulima wa kawaida anafaidika vilivyo kutokana na bidhaa hii, hapo mi ndio sasa naanza kuingiwa na wasiwasi juu ya hilo

Je ni huyu mkulima anayetumia jembe la mkono au ni yule ana anayetumia teknolojia katika kulima na kupanda halafu anayetengemea mvua ?

Au ni yule mkulima ambaye haitaji mvua anagharamika kutengeneza miundo mbinu ya umwagiliaji na anayetumia teknolojia ambazo kwa kawaida huwa wengi wao huenda wamechukua mkopo!

Mimi nimeshawahi kuishi Morogoro kama miaka mitatu hivi kwa kweli nilikua nikijionea mwenyehe jinsi jinsi magari yanavyoingia mashambani kununua mahindi mabichi

Katika maeneo hayo huwa wakulima hukadiria eneo kwamba kutoka hapa mpaka hapa utanoipa kiasi fulani bila kujali kuwa makadirio ya namna ile yeye anaweza kupunjwa na kazi aliofanya ni kubwa zaidi

Kumbumka mchoma mahindi unaemuona hapa mjini nakuuzia muhindi shilingi 250 na 300 na hata wengine huuza kwa 400 kwa muhindi moja

Ukifika katika masoko ya mahindi pale tandika au tandale utakuta muhindi mmoja huuzwaa kati ya shilingi 120 mpaka 170 au kwa wengine 200 pia huuza

Maswali mengi tunajiuliza huku tukiona kama mkulima atakuwa na hali ngumu kama sokoni hiyo ndio bei yeye atakuwa kauza kwa shilingi ngapi kwa kila hindi moja ?

Inawezekanna wewe ukawa shahidi namba mbili hata kwa kujionea jinsi magari yanavyomwagika kutoka mikoani yakiwa yamesheni mahindi mabichi kama hujaona tembelea masoko ya tandika au tandale ili uweze kuwa shahidi mzuri

Huko vijijini mi sijawahi kuona au kusikia soko kama haya ya hapa dar ambapo yanauzwa mahindi mabichi na bei zinazojulikana ,kama nikweli hakuna ni wazi kuwa mkulima mdogo anapunjwa na anahitaji ushauri nasaha

Wakati fulani wizara ya kilimo chakula na ushirika ilikaza uuzwaji wa mazo ya kiwa shambani kwa kuwa walilitambua hili na dawa ya kumsaidia mkulima ilikuwa ni kukazata ununuzi wa mazao yakiwa shambani

Mkulima atakapopewa labda laki mbili au tatu akauza mahindi yote alioko shambani huenda anaona zile ni pesa nyingi sana kwa kuwa zimekuja kwa pamoja na huenda labda kwa wakati ule alikuwa na shida

Lakini ukweli ni kwamba kama yale mahindi angeyavuna naamini angeweza kupata faida zaidi kuliko alichokifanya kwa muda ule

Kwani hata ukipiga mahesabu, gharama za kulima ,za kupand , kuhudumia mmea mpaka ukazaa na mpaka mteja akaupenda kuunuua kwa kiasi hicho utagundua kuwa gharama aliingia sio sawa na gharama aliouzia

Na hili ndio maana kila siku mkulima njaa kwake haishina kila siku serikali inawapa msaada , na sio kweli kuwa wanakosa kabisa ijapokuwa pia sio wote wanapata

Kama mkulima anaweza kupewa labda laki tatu au nne hawezi kuzitumia kwa muda wa miezi sita lakini kama hayo mahindi angeyavuna kwa utaratibu na kuyahifadhi vizuri angayeweza kuyauza kwa bei nzuri na kwa kipimo kinachoeleweka

1 comment: