Thursday, July 30, 2009

Monday, July 20, 2009

UBORESHAJI WA KILIMO

Na Bashir Salum

Wengi wetu tumekuwa tukiimba nyimbo lakini uchezaji wake hatujui tunachezaje kwa kuwa hata mlio wa mdundo wa ngoma yake hatuujui

Ni wazi sasa kuwa Wimbo tuliokua tunajifunza wote sasa tumeshaujua na kilichobaki sasa ni kujifunza namna ya kucheza kutokana na vionjo vya wimbo wenyewe ulivyo

Kwa kawaida kila wimbo una uchezaji wake na hivyo kama kila mtu atabadilisha wimbo ghafla basi ni wazi kuwa hata uchezaji nao utabadilika

Kwa kipindi kirefu kidogo wimbo wetu ulikuwa ni ‘vijana kukimbilia mjini’ wakitafuta maisha mazuri na yenye unafuu

Katika hatua hiyo wimbo ule tuliuimba lakini kwa kuwa hapakuwa na ngoma tukajikuta kila mtu anacheza kwa mtindo wake anaoufahamu yeye.

Vijana wakakimbilia mjini wakidai kuwa eti kilimo hakilipi wakidhani mjini ndio maisha bora yaliko


Kila mtu ana fikra zake lakini ni kweli kuwa mjini hakuna maisha yanayoshinda maisha ya kule kijini kama misisngi ya uchumi wa kilimo ikisimamiwa vizuri

Hii ilitokana na kuwa kuhamia mjini kwa vijana wengi kulifanya kilimo kikadumaa na wakulima wengi na wale maisha yao yanayotegemea kilimo wakaanza kubadilisha wimbo

Wakati kilimo kinadumaa lakini hata kikichangiwa na vijana wenye nguvu kukimbilia mjini hivyo kukosekana kwa nguvu kazi mambo yakabadilika na kukatokea kwa nyimbo mbili tofauti na kuanza kuimba ule wa ukitaka maisha mazuri yapo mjini

Vijijni kilimo kinasuasua ! huko mji nako vijana walikimbilia kazi ya kuuza nguo yaani wamachingalakini baadae wakijikuta wakilazimika kuimba wimbo mmoja na askari wa jiji yaani jeshi la mgambo

Wimbo wa mgambo huu sio wa kawaida kwani uliwafanya baadhi wa vijana kuukumbuka ule wa shambani ambao ulikuwa mrahisi hata kuucheza

Baada ya matatizo ya kila mtu kutaka kuimba wimbo wake ndio yaliosababisha watanzania waliowengi kuimba wimbo wa huzuni ijapokuwa hawakuwa wakiupenda

Wimbo huu wa huzuni unaimbwa na yeyote mtu si mtoto wala mkubwa wote wanaweza kuiimba nafikiri ni kwa sababu ya machungu yake

Vijana wazee watoto wakina mama wote wanauimba na kuucheza kwa ufasaha wimbo huu ulijulikana kama upungufu wa chakula

Kwa namna moja au nyingine mimi na wewe pia tuna lazimika kuimba wimbo huu hata kama sio ijapokuwa kuimba tu isingetosha kama hakutakuwa na kucheza wimbo huu

Kwa mara nyingi huwa tunaimba nyimbo ili tujifurahishe kwa maana wimbo huleta faraja moyoni hivyo wimbo unatakiwa kuleta faraja na wala sio kilio au huzuni

Wimbo huu wa upungufu wa chakula kutokana machungu yake ulimpelekea Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania aliponuia kwamba kilimo kikisimamiwa vizuri kitawafanya watanzania kuimba wimbo huku wakicheka badala ya kuimba wimbo huku wanalia

Mbali ya kutangaza bajeti ya kilimo kuongezwa katika mwaka wa fedha ujao lakini Mh. Rais pia alitoa kauli iliyoidhinishwa na bunge kuwa pesa zinazorudishwa kutoka katika akaunti ya madeni ya nje EPA zielekezwe katika kilimo na kwa wafugaji

Kauli ambayo imeanza utekelezaji na matunda ya kauli hiyo yameanza kuonekana kwa wakulima hasa wale wa Morogoro katika vijiji vya mkula na sehemu nyingine

Katika hali ya kukomesha wimbo wa huzuni yaani njaa katika taifa pia mheshimiwa Rais aliwaruhusu wafanya biashara kuingiza chakula kutoka nje bila kutozwa kodi ili chakula kupatikana kwa kiasi kikubwa na kuwafanya watu kununua kwa gharama nafuu

Katika mkutano wake na viongozi wa Wizara ya Kilimo uliofanyika Ikulu hivi karibuni Rais alisema kuwa wafanya biashara wanaruhusiwa kuingiza tani 300,000 bila ushuru wowote ndani ya miezi mitatu

Rais Jakaya Kikwete alisema hayo wakati wa kikao chake cha tathimini ya utendaji katika serikali alipokutana na viongozi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika

Katika jitihada zake za kukabiliana na tatizo la upungufu wa chakula nchini amewataka watafiti wenye nguvu lakini wamefika muda wa kustaafu kuendelea na kazi

Hatua hiyo ya kipekee inadhihirisha ni jinsi gani watu sasa wamechoshwa na wimbo wa huzuni wa kila siku kila mwaka na kila mahali

Kwangu mimi binafsi naamini kabisa kuwa kwa hatua hizo zingeweza kukibadilisha kilimo na kukifanya kisiwe cha kukimbiwa na vijana ambao kwa kipindi cha nyuma walijazana mjini wakipambana na mgambo wa jiji

Kwa hatua hizo ili ziweze kufanikiwa ni jukumu letu vijana tuache migogoro na mgambo wa jiji tikinyanganyana mashati na maji ya baridi kule mjini , turudi tukawekeze kwenye shamba uwezekana ni mkubwa sana kwa wakulima kufanikiwa

Nchi nyingi duniani ikiwemo china zilianzia kwenye jembe la mkono na katika kilimo cha familia kama Tanzania lakini wao sasa kilimo kimekuwa cha kibiashara kwa kuwa tu kiliweza kushirikisha vijana

Hayo yalisemwa hivi karibuni katika wizara ya kilimo chakula na mkurugenzi mtendaji wa China National Agriculture Development Group Coup Bank bwana Chen Youn

Wakati wakiingia mkataba wa ushirikiano katika kilimo na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ili kuharakisha mapinduzi ya Kilimo nchini Tanzania

Aidha bwana Yuan alisema nchi ya China imejipanga kikamilifu hasa katika kilimo na mifugo ili kuleta maendeleo katika sekta husika

Mkataba huo kati ya wizara ya Kilimo na benki kuu ya china inatuashiria sasa turudi shambani tukalima kwa maana Kilimo sasa kinamuelekeo thabiti

Jitihada za serikali hazikuishia hapo tu lakini kwa kipindi kifupi wizara ya kilimo iliingia mkataba na wizara ya mambo ya ndani na ikihusisha jeshi la magereza na lile la kujenga nchi
Hata hivyo mkataba huo ulifanyika kwa makusudikutokana na wanajeshi kuweza kufanikiwa sana kuzalisha mbegu bora na endelevu

Ni pale Rais alipotembelea viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma na kuwashauri wa tafiti wa mbegu wa Wizara ya Kilimo kuungana na wenzao wa jeshi la magereza na lile la kujenga taifa kwa kuwa wao wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuweza kubuni na kuendeleza mbegu bora

Zote hizo ni jitihada za serikali za kuhakikisha ule wimbo haumbwi tena katika nchi yetu ijapokuwa umezoeleka masikio na midomoni mwetu

Hata hivyo jitihada za kukiendeleza Kilimo hazikuishia hapo kwa Rais pia Waziri mkuu Mh Pinda mwaka jana alipokuwa katika mkutano na wakulima mjini Morogoro katika hoteli ya BZ alisonesha nia yake ya kuanzishwa kwa benki ya wakulima

Alisitiza ubora wa kuwepo benki ya wakulima kuwa itamuwezesha mkulimakukopa kiasi anachotaka na na kurudisha kwa riba ndogo

Jitihada hizo za Mh. Pinda zimeonekana kuwa na mafanikio makubwa ambapo uanzishwaji wa benki hiyo ya wakulima ipo katika hatua ya mwisho ya kuanzishwa

Inatarajiwa kuwa kufikia mwaka kesho yaan 2010 benki hii itakuwa tayari imekamilika na itaanza kutoa mikopo kwa wakulima kwa riba kidogo

Serikali ya Jamhuri ya watu wa korea kumbe nayo ilisikia ule nyimbo watanzania ambayo wanaimba huku wanacheka lakini wanalia kimoyomoyo

Ubalozi wa Korea ulioamua kuipa Tanzania zzana nyingi za kilimo kwa mkoa wa morgoro wakiwa wanatambua kabisa kuwa morogoro panategemewa kuwa ni ghala la chakula

Serikali ya jamhuri ya watu wa korea ilweza kutoa mashine mbili za kuvunia combine harvestertracto za kupanda mpunga mbili za kuendesha na za kukotwa kwa mikono ikiwa ni pamoja na pampu za maji

Hata hivyo wakorea hao waliweza kutoa matrekta 30 pale mjini morogoro kwa ajili ya kulimia kwa lengo la kuhimiza mapinduzi ya kijani

Msaada huo kutoka katika serikali ya Korea uliopokelewa na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Wasira mjini morogoro ulidhihirisha wazi kuwa sasa tunafanya Mapinduzi ya kijani

Jitihada hizo zote ninaamini vijana tukiamua kuachana na vurugu za mgambo wa jiji tukirudi mashambani tutakuwa na wimbo mmoja, tutacheza pamoja na vijana wa kisasa wanasema ‘kitaeleweka’

Ili kuweza kufanikisa haya katika kiwango cha mafanikio nilazima tuanzia kubadilika katika Kilimo cha umwagiliaji kwa maana ya kuachana na kutegemea mvua zetu hizi za msimu

Bila umwagiliaji hakutaweza kuwa na Mapinduzi ya Kilimo na pia wimbo wa njaa utaendelea kuwepo daima hivyo ni jukumu letu mimi na wewe tujiandae kukopa katika asasi tofauti zinazokopesha ili tuwekeze katika Kilimo

Wapo vijana ambao wameweza kunufaika sana kwa kupitia kilimo na kunufaika na sasa wanaendesha maisha yao vizuri
Hata Balozi wa Japani nchini Hiroshi nakagawa alipokuwa akizungumza alipozungumzia kuhusu sekta ya Kilimo hasa cha umwagilaji katika mkutano wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika (TICAD) aliligusa sana kilimo cha umwagiliaji hasa kwa Tanzania

Alilisitiza kuwa Kilimo cha umwagiliaji ndio kilicholeta mafanikio makubwa nchini kwake ambapo Tanzania ikiaamua kufanya mabadiliko

Mwisho

Tuesday, July 14, 2009

MKOA WA KILIMANJARO NJAA KILA WAKATI

Na Bashir Salum

Watu husema umaskini ni sawa na mzigo wa mzoga ambao kama hutautua kwa ajili ya harufu yake basi utautua kwa uzito wake.

Haya ndio yanayowakuta watu watanzania wengi hasa wa Mkoa wa Kilimanjaro ambao wana mzigo wa upungufu wa chakula kwa sababu ya kutegemea mvua za msimu.

Mkoa wa Kilimanjaro unatakiwa kutumia mbinu za ziada ili kuutua mzigo wa upungufu wa chakula unaoikabili mkoa ule hasa wilaya ya Mwanga mara kwa mara .

Upungufu wa chakula unao ukumba mkoa wa Kilimanjaro unaweza kuzuiliwa kwa kuboresha kilimo, ufugaji na kuvitumia vizuri vyama vya kuweka na kukopa.
Vipo vyama vingi vya kuweka na kukopa vilivyoanzishwa na wananchi wenyewe lakini hata wakopaji wamekuwa wakiitumia katika kilimo ambacho nacho hutegemea mvua za msimu

Ni sababu hiyo ya utegemezi wa mvua ndio maana hata mikopo hiyo inakuwa haiwasaidii sana katika kuondoa kawaida ya kuwa na njaa za mfululizo

Kutokana na kutegemea mvua za msimu wakulima mkoani Kilimanjaro wamekuwa wakishindwa kupata mavuno ya kutosha kutokana na uhaba wa mvua ambao kwa kipindi hiki umekuwa ukijitokeza kwa kiasi kikubwa.

Wakulima wadogowadogo inafaa wawe wanatafuta pembejeo za kilimo kulingana misimu waliyonayo mkoani Kilimanjaro.

Naibu waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Dr David mathayo alisema njia inayoweza kumhakikishia mkulima kuwa na uhakika wa chakula katika mikoa ile ni kujikita katika kilimo cha umwagiliaji, uchaguzi wa mbegu bora katika upandaji na kuwa na kawaida ya kuhifadhi chakula

Mbegu za mda mfupi na zenye kutoa mazao mengi pia mazao yanayovumilia ukame kama mihogo na mtama yapewe kipau mbele kwa wakulima wa mkoa wa Kilimanjaro ili yaweze kuondoa upungufu wa chakula

Mkurugenzi wa Idara ya usalama wa chakula , Bwa John Mgodo amesema kuwa mikakati shirikishi imeandaliwa kuhakikisha kuwa chakula kilichopo kinawatosheleza wahitaji hasa mikoainayoweza kukabiliwa na njaa

Wakulima wengi mkoani hapo hutegemea kilimo cha mvua na wachache sana kutegemea kilimo cha umwagiliaji ambacho hupatikana zaidi katika sehumu za tambarare kwa msaada wa maji yatokayo kwenye misitu mbalimbali kama vile shengena, kindoroko na mlima kamwala na ile ya mlima Kilimanjaro

Pia ardhi ya sehemu kubwa ya mkoa huo imechoka sana kutokana na kulimwa kwa mda mrefu bila ya mbolea na hata kuongezeka kwa idadi ya wakazi na shughuli nyingine za kimaisha

Hivi karibuni nilikuwa Mkoani Kilimanjaro katika wilaya ya Mwanga nilikutana na mzee mmoja aitwae Sawaya Mchwangondo Marisa (85) wa Usangi Vuagha aliweza kunieleza yafuatayo

Kumekuwa na utamaduni wa aina yake katika upatikanaji wa mvua na upatikanaji wa mavuno na kutokea kwa njaa hasa katika wilaya ya mwaga

Historia inaonesha kuwa Mkoa wa Kilimanjaro kila mwaka unaoshia na 4 au kugawanyika kwa nne lazima kuwepo na ukame pamoia na njaa ambayo huathiri sana uchumi wa Mkoa wa Kilimanjaro

Mwaka 1964 Mkoa wa Kilimanjaro ulikumbwa na njaa ambayo wakazi wa mkoa huo hususni wapare waliita njaa ya mkebe (nzota ya mngebe) kutokana na vyakula vya msaada kupimwa na chombo kiitwacho mkebe

Mnamo mwaka 1968 ilitokea njaa lakini ilikuwa sio njaa kubwa kuliko ile iliotokeo mwaka 1974 ambayo chakula kilichokuwa kinapatikana ni mihongo na yenyewe ilikuwa inapatikana kwa uchache zaidi

Lakini hata hivyo kuanzia mwaka 1978 hali ya chakula ilikuwa sio nzuri ijapokuwa watu wachache wategemeao kilimo peke yake waliathirika zaidi kutokana na mavuno kupatikana lakini yalikuwa kidogo yasiokidhi haja za wakulima

Mwaka 1984 imeelezwa wazi kuwa upungufu wa chakula ulitokea Mkoani Kilimanjaro ulikuwa ni wa kutisha katika kipindi chote ambacho njaa ilshawahi kutokea

Serikali ya kipi hicho cha mwalim Juliasi Nyerere ulichukua hatua za kuaagiza chakula kutoka nje kilichojulikana kama mahindi ya Yanga (yalikuwa ya njano)


Kwa kipindi hiki Taifa zima halikuwa na chakula cha kutosha hivyo haikuwa mkoa wa Kilimanjaro peke yak e bali mikoa yote iliguswa na tatizo alisema mzee sawaya

Imekuwa kawaida watu wa mkoa huo kuamini kama kila mwaka utakao kuwa unnaishia na nne au nane kwao itakuwa na uhaba wa chakula hivyo mwaka uliopita 2008 kwa ujumla wake mkoa wa Kilimanjaro haukuwa na chakula chakutosha kabisa

Upungufu wa chakula mkoani Kilimanjaro huwa unasababishwa zaidi na ukosefu wa mvua za uhakika katika kipindi kizima cha mwaka na kutokuwa na mikakati ya kuhifadhi chakula.

Hata kiwango cha maendeleo kilichofikiwa na Mkoa wa Kilimanjaro kama ujenzi wa nyumba mashule, hoteli na miundo mbinu bora huwa ni moja ya mambo yanayochangia uharibifu wa mazingira yanayochangia kuchoka kwa aridhi mkoani humo

Kutegemea kilimo cha mkono kwa wananchi wengi mkoani pale ni moja ya sababu zinazofanya kutokea kwa upungufu wa chakula ambao hurudisha nyuma kasi ya maendeleo mkoani hapo.

Wakulima wengi wamekuwa hawatumii mbegu sahihi ambazo hazijahakikiwa na wataalamu kwa ubora hivyo kufanya mkulima kutopata mazao ambayo yangemtosheleza katika maisha yake

Tunasema kuwa hali chakulamtu wa kawaida mkoani humo debe moja la mahindi ni 7000 na 8000 sawa na 350 na 400 kwa kilo

Jitihada za makusudi katika hili ni muhimu zichukuliwe ili kuondokana na matatizo ambayo yanaweza kuwa sio ya lazima kwa kuwa inawezekana

Jitihada inayofanywa na ASDP ya kuwawezesha wakulima kupitia ngazi ya wilaya ya DADPS katika kujenga uwezo wa kujiwezesha

Wananchi wa mkoa huo wanatakiwa kutumia mfuko huo wa ASDP katika kuibua miradi mbalimbali ili aweze kupanua uwigo wa upatikanaji wa chakuala na kufanya maisha kuwa marahisi

Mfano katika vijiji vya kata ya Jipendea ambapo hupata maji kutoka sehemu za milimani ikiwemo Usangi, Ugweno na Kilomeni wangeweza kutumia ile asilimia 75 ya uwekezaji inayotolewa na serikali na wahisani kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji

Ipo haja ya technologia za kilimo utumiaji wa zana za kisasa na utaalamu wa kumwagilia kwa kutumia mabomba kutokana na kutumia maji kidogo

Ijapokuwa kunawafugaji ni wengi mkoani Kilimanjaro lakini wanategemea kilimo zaidi ya ufugaji kutokana na shughuli za mifugo kutouwa na tija

Kiasi hicho hakiwezi kuhudumia mahitaji ya familia kama chakula, mavazi,ada ya shule na kujitibu upatapo magonjwa kwa muda wa mwaka mzima

Mifugo inayopatikana mkoa wa Kilimanjaro haiwezi kuondoa njaa kutokana uhaba, na udhaifu wa mifugo yenyewe

Ukame unapo tokea sehemu husababisha Mazao ya chakula kuwa na bei ya juu, mazao mengine ka mifugo yanashuka bei kutokana na ukosefu wa pesa na malisho kwa mifugo

Kwani ukame husababisha mifugo kufa au kukosa afya hivyo kuuzwa kwa bei ya chini ili kukwepa kuwapoteza kabisa

Hivyo ukame unapotokea sehemu Fulani ,mifugo haiwezi kuondoa njaa kwa sababu hata yenyewe huwa inaathirika na ukame na hivyo soko lake linapungua

Hata hivyo wafugaji wengi wa mkoa wa Kilimanjaro hawajawezeshwa kufuga il kupata manufaa ya mifugo yao lakini wao hufuga kama sehemu ya utamaduni wao

Mifugo yao mingi haipatiwi chanjo za magonjwa na hawana elimu ya ufugaji wa kitaalamu ambao ungewawezesha kupata manufaa ya ufugaji

Ili wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro uondokane na njaa za mara kwa mara mbali ya kushiriki kilimo cha umwagiliaji wanatakiwa kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa ili kupata mitaji na kuboresha mifugo yao ikiwa ni pamoja nakupata chanjo za mifugo yao

Mkoa wa Kilimanjaro ni mojawapo ya Mikoa ambayo ina wasomi wengi kuliko Mikoa mingine wataalamu hawa wanatakiwa kushirikiana na kuwashauri na kutoa utaalamu wao ili kuondoa tatizo hili ambalo limekuwa likijirudia kila mara

Katika Tarafa ya Usangi Mkoani Kilimanjaro msimu wa maharage huvunwa kwa kiasi kikubwa lakini wakulima huyauza, tena kwa gharama ndogo, hivyo Serikali za Mitaa zisimamie uuzaji wa mazao ya chakula kiholela ili kuhifadhi chakula cha akiba

Hata hivyo Mbali ya ushirikishwaji wa wananchi katika kilimo cha umwagiliaji na mikakati mingi ya kuhifadhi chakula kwa ajili ya matumizi ya baadae serikali pia inahakikisha kuwa pembejeo za kilimo, dawa na ruzuku kwa wakulima vinawafikia kwa muda unaotakiwa

Mbali na hali ya chakula ambayo inaonekana kwa mwaka huu haitakuwa nzuri Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliwaambia wananchi wakatia akihutubia wananchi wa unguja na pemba alisema kuwa hakuna mtu atakaye kufaa kwa ajili ya njaa

Hii ni kutokana na ukweli kwamba katika akiba ya taifa yaani yale maghala ya kuhifadhi chakula bado kuna chakula cha kutosha hapa nchini

UKOSEFU WA CHAKULA UMEZIKUMBA WILAYA NYINGI HAPA TANZANIA

Na Bashir Salum,

Umaskini sio tatizo bali ni changamoto katika maisha haya ni maneno yaliosemwa na mtaalamu mmoja wa mambo ya uchumi kutoka nchi za magharibi

Haya yanatokana na mtu hujifunza kutokana na makosa hivyo umaskini tukiuchukilia kama kosa litatufanya tutafute namna ya kutolirudia kosa

Unaweza kutumia nafasi ya umaskini ulionao ikawa kama changamoto za kimaisha na ukakuletea ubunifu na ukaepukana na umaskini daima

Wanauchumi husema kuwa katika uzalishaji lazima uangalie kiwango cha rasilimali ulichonacho ndipo ufanye uchaguzi sahihi kutokana na rasilimali zilizopo

Ukosefu wa chakula unazikumba wilaya ya nyingi hapa nchini unaweza kuzuiliwa au kutokomezwa kwa kuangalia misingi ya kiuchumi na kimazingira yaani rasilimali zilizopo

Rasilimali zikitumika vizuri sisi watanzania wimbo huu wa uhaba wa chakula ulioanza tangu mimi sijazaliwa ndipo utakapoweza kupata mwitikiaji

Kama uionavyo foleni ya magari katika jiji la Dar es salamu kila kukicha ndivyo ilivyopanga foleni njaa na kujisogeza kidogokigogo katika maisha ya mwanadamu wa kitanzania

Kutokana na ukame unaozikumba wilaya nyingi hapa nchini zinatakiwa mbinu mbadala za kuweza kuhakisha kuwa foleni hii ya njaa toka mwaka 1961 mpaka huko tuendako inapatiwa dawa

Asilimia zaidi ya 80 ya maisha ya mtanzania yanategemea kilimo lakini pia sio lazima asilimia 80 ya chakula cha mtanzania kitokane na kilimo

Zipo sekta nyingine zinazoweza kumfanya mtanzania akapata chakula katika njia tofauti na kilimo kuliko kutegemea kilimo cha kutegemea mvua

Serikali kupitia matawi yake kama wizara ya kilimo inafanya mambo mengi ikiwa ni jitihada zake za kuwaepusha wananchi na matatizo ya ukosefu wa chakula nchini kote

Hii ikiwa ni pamoja na kuanzisha program mbalimbali zikiwa na sura ya (MKUKUTA) yaani mkakati wa kupunguza umaskini japo haijafikia asilimia zilizotzrajiwa

Mbali na jitihada zilizofanywa na serikali lakini Imeripotiwa kuwa mikoa ya Kilimanjaro, Tanga , shinyanga na mkoa wa Mara zimekuwa na matatizo ya upungufu wa chakula

Mkoa wa Singida unahitaji jumla ya ya tani 309 za chakula ili kukidhi angalau kwa kiasi kidogo hali ya mbaya ilijitokeza hivi karibuni

Hayo yalisemwa na mkuu wa mkoa wa Singida Bw Parseko Kone wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya serikali ya mkoa huo kwa waandishi wa habari

Hata hivyo bwana kone alisema kuwa maeneo hayo ambayo yameainishwa yapo katika ukanda wa bonde la ufa katika wilaya ya Manyoni na Iramba

Pamoja na hayo wilaya ya manyoni kuna upungufu wa tani 247zinazohitajika ili kuondoa tatizo la njaa lilowakumba wakazi wa eneo hilo

Katika wilaya ya Iramba ya katika mkoa wa Singida inahitaji tani 62 za chakula na hivyo kufanaya jumla ya tani zinazohitajika kufikia 309

Tukiangalia katika Wilaya ya Same yenye zaidi ya wakazi Wilaya ya Same ambayo inawakazi zaidi ya 244,089 baadhi ya yao wanakumbwa na uhaba wa chakula

Zaidi ya wakazi 30,000 wa kata 15 za wilaya ya Same wanahitaji chakula cha msaada kutoka serikalini

Kwa mujibu wa afisa kilimo na maandeleo ya mifugo na kilimo wa wilaya hiyo Majid Kabyela amesema tani 764 za chakula zinahitajika ili kuwanusuru wakazi hao na baa hilo
Maeneo ya liothirika ni kata ya Mhezi,Myamba, Msindo, Kisiwani Vunta,Hedaru, Suji, Makanya , Vudee, Mwembe, same, Njiro, na Kirangare

Tathimini iliyofanywa septemba mwaka jana ilionesha kwamba wilaya 20 wangeweza kukabaliwa na upungufu wa chakula katika mwezi wa disemba mwaka jana na mwezi huu hivyo kuhitaji tani 7182 za chakula ambacho tayari kilishatengwa kutoka (national food reserve agency) NFRA

Hata hivyo Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu (sera uratibu na bunge) Philip Marimo baada ya kutembelea ghala la hifadhi ya chakula la kipawa Dar es salam alisema kuwa baadhi ya wilaya zimeshatengewa fedha ya kuweza kusafirishia chakula hadi vijijini

Moja ya wilaya zilizopata kutengewa hela ya kusafirishia chakula kitakachotolewa na serikali ni Bunda, Iramba, Manyoni, Rombo, Mwanga, Same, Monduli, Ukerewe, Bariadi, Kishapu na Shinyanga vijijini

Wakati huo imeripotiwa katika gazeti la Tanzania daima la tarehe 26 januari kuwa zaidi ya wakazi 300 wa kijiji cha Kalalani wilayani Korogwe wapo hatarini kupoteza maisha kutokana na njaa inayowakabili

Taarifa hiyo ilizibitishwa na serikali ya kijiji cha Kalalani ni kwamba eneo hilo linalokumbwa na janga la njaa na msaada wa haraka unahitajika ili kuhakikisha kuwa maisha ya wakazi hao yananusurika

Hii ikiwa ni moja ya jitihada inayofanywa na serikali kufanya tathimini na kuyatambua maeneo yalio na upungufu wa chakula na ili kuweza kutatua matatizo yalioko

Hata hivyo haya yanaendana na kauli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alitoa akiwa visiwani Zanziba kuwa hakuna mtu atakaye kufa kutokana na njaa

Mimi tokea nasoma shule ya msingi nilikuwa nikisiki mkoa wa Dodoma kunakuwa na uhaba wa chakula lakini kumekuwa na jitihada za makusudi mji ule

Katika sikuku ya nanenane ya mwaka jana iliyofanyika kitaifa viwanya vya nzuguni mkoani Dodoma mwenyeji alukuwa ni mkuu wa mkoa wa Dodoma bwana Lukuvi

Bwana Lukuvi alisema kuwa mkoa ule unafanya jitihada za hali ya juu kuhakikisha kuwa inatumia rasilimali zake ili kuondokana na kuhakisha kuwa mkoa unajitegema kwa chakula

Enzi za mwalimu ambapo inawezekana mi nilikuwa mdogo lakini nilipata kuelezewa kuwa mwalimu alikuwa mkali sana kwa upande wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya hasa katika kuwa karibu na maendeleo ya mikoa yao

Moja kati ya hadithi nilizopata kuzisikia ni kuwa mwalimu alishawahi kusema kuwa ‘tunaweza tukafukuza mabwanashamba wote na kilimo kikaendelea kuwa hai’

Kwa kauli hii ya mwalimu ni kwamba inawezekana kuwa mabwanashamba wapo lakini hawafanyi kazi ndio maana hakuna tofauti na wasipokuwepo

Mimi siemi hivyo lakini niseme tu kuwa ni vizuri mabwanashamba kufamu kuwa mkulima anayetegemea kilimo akilia njaa hayo yatakuwa ni mapungufu ya bwanashamba husika

Pamoja na hayo turudi kwenye ukweli kuwa Tanzania inayojivunia mbali tu kilimo lakini bado kuna rasilimali nyingi ambazo zipo na zingeweza kuwa mbadala hasa kwa nia ya kuondoa upungufu wa chakula

Hivi ukifikiria kwa makini mkoa wa Kilimanjaro wenye vivutio vingi, mkoa unaoitambulisha Tanzania duniani mkoa unaunganisha Tanzania na nchi za jirani kama Kenya na ni mkoa wenye misitu midogo na mikubwa lakini eti wanalia njaa?

Ukiangalia mkoa wa Tanga hautataja historia ya Tanzania bila kuutaja mkoa wa Tanga mkoa ulio na bandari na tena mkoa wenye vivutio vya kila aina na ardhi yenye rutuba na unaunganiasha mji muhimu ya Tanzania ikiwemo Dar es salaam na Arusha lakini leo korogwe wanalia njaa!

Ukiangalia mkoa wa Mara nao una utajiri mbali na kuwa una uwezo katika kilimo lakini pia ni mji wa kitalii na kibiashara zaidi
Ni lazima maisha ya mtanzania yaangaliwe kwa jicho la tatu na maisha yasipelekwe ki siasa yawe kivitendo

Kuanzia ngazi ya kijiji hadi ngazi ya mkoa kuwepo na mshauri katika mambo ya maendeleo na kujihami kutokana na kubadilika kwa hali ya nchi

Kila mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya na halmashauri zake angetakawa kuwa wabunifu na kuweza kuzitambua rasilimali mbalimbali zinazopatikana katika mikoa au wilaya hizo ili kuondokana na aibu hii ya njaa

Angalia mkoa wa Mara,Kilimanjaro,Tanga na hata Singida utagundua kwamba kuna rasilimali kubwa katika mikoa hiyo ambayo ingetumiwa vizuri njaa haitakuwepo

Ni kweli kabisa kuwa tunategemea kilimo lakini kuna sekta nyingine ambazo zinasapoti sekta ya kilimo na zinaweza kuwafanya watu kupata chakula cha kutosha mbali ya kilimo

Lakini hata kutumia zile fursa za ASDPS na DADPS ili kuzindua miradi mingine ambayo itasapot kilimo kwa kupata kipato zaidi bila kuuza mazao yetu ya kilimo

Ili wilaya hizi ziweze kuondokana na foleni ya njaa ni lazima kuwepo na mkakati wa kutumia maligafi zote ambazo zinapatikana ndani ya wilaya hizo badala ya kutegemea kitu kimoja

Hata hivyo Kama kilimo cha umwagiliaji kitapewa kipau mbele kwa maeneo ambayo yanayobahatika kupata maji yanaweza kuondoa tatizo la njaa kwa kuendeleza umwagiliaji

Eidha kupunguza biashara ya mkaa na upasuaji wa mbao kunaweza kusaidia kuondoa tatizo la ukame na njaa kwani uchomaji wa mkaa umechangia kuongezeka kwa ukame katika wilaya ikiwemo same mwanga na zinginezo

Kutilia mkazo vyama vya ushirika nayo ni nyenzo muhimu katika hili kwani ushirika unaweza kutoa huduma za pembejeo , na mikopo na masoko ya mazao kwa wananchi na pia kufanikisha mipango ya maendeleo

Elimu ya ujasiria mali ni muhimu pia kwa watu wa mikoa na wilaya zilizoathirika na baa la njaa kwa sababu sio lazima kutegemea kwenye kilimo na biashara ya mkaa tu bali unaweza kupata elimu ya ujasiria mali waweze kutumia malighafi chache zilizopo kwa manufaa

Mihogo ambayo inapatikana katika wilaya ya Same mwanga na hata baadhi ya wilaya za mkoa wa mara kama elimu ya ujasiria mali itawafikia wanaweza kujua kwamba zao hilo mbali ya ugali unaweza kutengeneza vitu vingine kama chapati, keki tambi na vituvingine ambavyo vingeweza kuondoa umaskini na utegemezi wa kilimo zaidi

Kama Serikali inavyo jitahidi kuanzisha miradi tofauti ya maji na kilimo cha umwagiliaji wilayani wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya waboreshe mali gafi ambazo zipo na zinaweza kuondoa matatizo ya chakula

Kwa yale maeneo kame kuwepo na utumiaji wa maji ya matone mfumo huu unatumia maji kidogo ukilinganisha na umwagiliaji wa mifereji ambao hutumia maji mengi katika kilimo

Naona sasa ifikie mahali iwe ni wimbo wetu wote kwamba wote tulime kilimo cha kisasa,na tutumie zana bora mbegu bora ili kupata kilichobora zaidi

Pamoja na hayo watanzania wote tuamue kufanya kazi tuwe wabunifu kwani matatizo sio kama upepo unavuma ambao mungu anauleta na hakuna binadamu anewezakuusimamisha

Matatizo yote yanaweza kwisha kama watu tukiwa na nia kuwa na moyo wa kujitolea na kuacha siasa katika kazi ila vitendo kwa wingi

Kuna msemo wa china unaosema kwamba ‘kizazi hiki kipande miti ili kizazi kijacho kipate kivuli’ tukiuamini na kuufanyia kazi msemo huu tutaondokana na matatizo kama haya

Hivyo tunatakiwa kujua kuwa hata siku moja Serikali haitamuwekea mtu pesa mifukoni mwake ila imeanzisha SACCOS ambapo mtu unaweza kukopa na kuendeleza shughuli zako

Sasa viongozi wetu ni lazima tutilie mkazo ushirika ilituweze kufaidika kupitia ili kuweza kufaidika kwa hilo

MWISHO

MICHE BORA YA MATUNDA ILIYOBEBESHWA

Umuhimu wa Miche Bora ya Matunda iliyobebeshwa Katika Kupunguza Umaskini

Matumizi ya miche bora iliyobebeshwa kwa kilimo cha matunda ni moja ya teknolojia muhimu itakayowawezesha wakulima kuongeza tija na kujikwamua kutoka katika umaskini.

Haya yanatokana na ukweli kwamba, miche iliyobebeshwa kitaalam huzaa matunda bora na mapema na hivyo humhakikishia mkulima mavuno bora na kipato cha haraka kuliko miche ya kienyeji.

Hayo yalisemwa na Afisa Kilimo Mwandamizi Bi. Judith Kitivo, mtaalam wa mazao ya bustani alipotembelewa ofisini kwake hivi karibuni.

Aidha, ubebeshaji wa miche ya matunda hufanywa kwa mazao ya jamii moja kwa mfano limau na aina nyingine ya limau, limau na chungwa au aina moja ya parachichi na nyingine alisema Bi Kitivo.

Hata hivyo, alizitaja faida nyingi zitokanazo na ubebeshaji wa miche zikiwa ni pamoja na kuharakisha uzaaji wa matunda kutokana na kukomaa kwa kikonyo kinachotumika, kudhibiti magonjwa na wadudu walioko udongoni, kupata miche yenye sifa nzuri, kuzalisha mazao miti (woody plants) ambayo hayawezi kuzalishwa kwa vipande (cuttings) pamoja na kuweza kuzalisha aina tofauti za mazao kama machungwa na limau katika mti au mmea mmoja; alisema mtaalam huyo.

Mbali na hayo alisema zipo aina mbili za ubebeshaji, ambazo ni ule wa kishina na kitawi /kikonyo (grafting) ambao hufanyika kwa uzalishaji wa miche kama miembe na miparachichi; na aina ya kishina na jicho la kikonyo (budding) ambao hufanyika kwa uzalishaji wa miche jamii za michungwa.

Monday, July 13, 2009

Maembe ni utajiri uliolala

Na Bashir Salum
Waswahili husema eti rizizki ya Mbwa ipo miguuni mwake,usemi huu unamaana kuwa riziki ya mtu ipo katika nafasi aliyo nayo na uwezo alionao

Maembe yaliopo Tanzania yanaweza kubadilisha na kumuongezea riziki ya mkulima wa Tanzania kama akielimishwa vizuri kuhusu ukulima bora na wa kisasa

Maembe yanaweza kumnyanyua mkulima kwa kumuongezea kipato na kuboresha maisha ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa nchi.

Utayarishaji wa shamba la miembe,mkulima anashauriwa kuandaa shamba mapema, kutumia mbegu na miche bora iliyofanyiwa utafiti na vituo vya utafiti hapa nchini.

Mikoa yote inalima miembe ila inatofautiana kwa kiwango cha uzalishaji kutokana na tofauti za maeneo hayo

Zao hili linalimwa katika mikoa yote kwa sababu ya uwezo wake wa kustawi katika aina mbalimbali za udongo na kustahimili aina mbalimbali za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na ukame.

Miembe inaweza kustawishwa mahali ambapo aina nyingine nyingi za mazao haziwezi kustawi.

Zanzibar ilishazalisha jumla ya Tani 6,546. Kiasi hicho cha embe kilivunwa katika mashamba yenye jumla ya eneo la Hekta 1,372

Ingawa miembe imepandwa Zanzibar katika eneo lenye jumla ya Hekta 1,734 na kaya zilizohusika na kilimo hiki ni 12,819.

Ingawa takwimu hizo hazikuonesha kuwa sasa Tanzani iko nafasi ya ngapi katika uzalishaji wa zao la embe ,

Hata hivyo zinaonesha kuwa kuna ongezako la Tani 146,028 katika kipindi hicho. Ambapo maembe mengi yamezalishwa hapa Tanzinia

Soko la maembe limekuwa kwa kiasi kikubwa duniani ikiwa ni moja ya sababu ya kuongezeka wataalamu wa maembe

Kuna aina zaidi ya 140 za embe ambazo hupatikana hapa tanzania na duniani kwa ujumla kulingana na mazingira yake
.
Ubora wa embe unatofautiana kutokana na sifa za embe na aina ya embe husika ijapokuwa kila embe lina ubora wake.

Sifa hizo zipo nyingi sana, hata hivyo ili kurahisisha kuzitofautisha baadhi ya embe zinazojulikana zaidi katika masoko Tommy Atikns KEITT na kent zill aina hizi ni nzuri sana

Hukomaa mwanzoni hadi katikati ya msimu Matunda yake ni makubwa, huweza kufikia kati ya gramu 450 hadi 700 Umbile la tunda ni kati ya umbile la yai na mviringo
Likikomaa huweza kukaa muda mrefu bila kuharibika Tunda lina rangi nyekundu ambayo haijakolea na imechanganyika na njano na Lina utamu wa kadiri

Zipo aina nyingi za maembe zilimwazo na wakulima hapa nchini kama vile embe dodo, bolibo, sindano, zafarani, mviringa na nyingine nyingi ambazo tumezizoea.

Aina hizo za maembe uzalishaji wake ni mdogo lakini wataalamu wameweza kuingilia kati tatizo la uzalishaji mdogo kwa kutumia mbinu ya ubebeshaji wa maembe.

Ubebeshaji wa maembe ni njia sahihi katika kuhamisha sifa halisi cha maembe kutoka kwenye mche unaotoa mavuno mengi bila kuathiri sifa na tabia za embe unalokusudia kupata.

Mbinu hiyo hutumia shina mama lenye sifa ya kutafuta chakula kwa wingi ardhini na hubebeshwa na aina nyingine inayokidhi mahitaji ya mkulima kwa kumpa bei nzuri.

Matokeo ya utumiaji wa mbinu hiyo ya ubebeshaji wa maembe sasa kuna aina mpya za maembe zinazoweza kupenya soko la maembe la kimataifa.

Aina hizo ni Red, Apple, Alphoncal ambazo tayari zimepiga hodi kwa wakulima wa maembe wa wilaya ya Mkuranga.

Mbali na hayo kuna aina ya miembe inayokidhi sifa hizo ni pamoja na Kent, Keith, Tommy Atkins, Alphonso, Sabre, Van Dyke, Apple, Ngowe na Red Indian (Zill).

Wakulima walio karibu na bustani zinazomilikiwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika pamoja na zile zilizoko chini ya manispaa wameanza kupanda aina mpya za maembe.

Bustani zinazomilikiwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kupitia kitengo chake cha promotion ya mazao zipo Mpiji wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani,

Bustani ya Manispaa Ilala yenye aina mpya za maembe ni ile ya Kinyamwezi ambayo ipo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kupitia Gongola Mboto kuelekea njia ya Chanika,Pia zipo nyengine ambazo zipo maeneo ya Lushoto na Muheza Tanga

Wakulima wengi hawajui kanuni bora za kilimo cha maembe na hivyo kuwafanya wakulima kutoyaona manufaa ya maembe

Tatizo kubwa linalo kabili uendelezaji wa zao la embe ni kutopatikana kwa miche ya kutosha ya miembe bora.
Pia bei kubwa ya miche ambayo, huuzwa kati ya shilingi 2,000/= na 3,000/= kwa mche

Ili kuondoa tatizo la upatikanaji wa miche bora ya miembe Wizara ya kilimo chakula na ushirika imeweka mkakati wa kuongeza uzalishaji wa miche hiyo na upatikanaji kwa wakulima.

Miche hiyo bora ina sifa za kuzaa maembe mengi kwa eneo na yenye ubora unaokubalika katika masoko yetu ya humu nchini na yale ya nje ya nchi.

Wapo wakulima ambao wanawezeshwa kuanzisha mashamba ya miembe bora kwa kupewa miche bora ya miembe na kupanda katika mashamba yao.

Miembe imepandwa katika mikoa ya Pwani, Morogoro na Dodoma na sehemu nyingine hapa nchini.

Mashamba hayo yanakuwa ni mashamba ya mfano ambapo wakulima wanayatayarisha mashamba kwa kufuata kanuni zote za kilimo bora cha miembe.

Mashamba hayo yatakuwa ni sehemu ya kuwafundishia wakulima wengine kwa kuona aina mbalimbali za miembe bora jinsi inavyoweza kuzaa maembe yenye ubora zaidi

Baada ya miaka mitatu miche hiyo itaanza kuwa tayari kutoa vikonyo ambavyo vitatumika kuzalisha miche mingine unaofanywa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika katika kuendeleza zao la embe.


Jumla ya miembe bora 5,141 imezalishwa na kupandwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili kuwafaidisha wakulima

Miche 595 ya miembe bora imepandwa Dodoma Vijijini huko Chamwino katika Tarafa ya Mvumi na vijiji vake, Makulu miche 200, Ilolo miche 100, Muungano miche 100 na miche 195 ilipandwa Ikowa Dodoma.

Pia Miche 150 imepandwa katika Kituo Cha Amani kijiji cha Makang’wa Dodoma,Miche 120 na kijiji cha mwambaya wilayani Mkuranga

Pia wapo wkulima ambao watagaiwa Miche mingine 400 wilayani Mkuranga namiche 250 itakayo gaiwa Morogoro.

Hata hivyo jumla ya Miche 3,500 ya miembe bora imezalishwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushika kwa kushirikiana na wanachama wa Chama cha Wakulima wa Miembe ili kuwanufaisha wakulima

Miche hii ya kisasa inachukua miaka miwili na nusu kuanzia kupanda hadi kuzaa ile ya zamani inayochukua miaka mitano had saba kupanda hadi kuzaa

Kila mwaka idadi hiyo ya miche itakayozalishwa itakuwa inaongezeka kwa zaidi ya mara mbili Mashamba hayo ni ya wakulima wenyewe ambapo yanakuwa na malengo makuu matatu yafuatayo


Kama wakulima watatilia mkazo kwenye zao hili kwa kutumia mbegu sahihi za maembe zinazo zaa sana na kuchukua mda mfupi wanaweza kuondokana na umasikini

Mkoa wa pwani hivi karibuni uliweza kujionea mradi wa maembe ulikuwa umetembelewa na Raisi Jakaya Kikwete unaomilikiwa na Dkt. Salum Diwani

Shamba lililokuwa limesheheni miembe mingi ya kisasa iliyokuwa imezaa vizuri ilikuwa ni changamoto kwa yeyote alikuwepo kwenye mkutano huo kulima maembe

Iliwekwa wazi kuwa soko la maembe hayo linapatikana nchini Tanzania na nchi za jirani kulinga na ubora wake

Raisi Jakaya Kiwete alitoa changamoto kwa wizara ya kilimo chakula na ushirika kuandaa program maalum kuendeleza kilimo cha maembe katika mikoa inapostawi

Ilikadiriwa kuwa mti mmoja mkubwa wa mwembe huweza kutoa maembe hadi 3000 na midogo hutoa maembe 300

Huu ni utajiri kwani mkulima akilima miti kumi ikazaa vizuri midogo inaweza kuzaa maembe elfu tatu 3000 na mikubwa kutoa maembe elif thelathin 30,000

Hivyo mkulima akiuza embe moja kwa shilingi 300 huweza kupata kati ya 900’000 na 9,000,000 kwa miembe mikubwa na midogo

Mkulima angeweza kufaidika sana na kilimo cha maembe na hata kuitambulisha nchi kimataifa

Kuna mradi ujulikanao kama common Fund for Commodity ambao Tanzania na Zimbabwe ni wanachama na wamepewa furusa ya kuandaa mazao ya biashara ya kuuza nchi za nje

Soko la miembe hapa Tanzania lipo isipokuwa wanunuzi kutoka nje wanahofia kufanya biashara na watanzania kwa kile wasemacho kuwa hawjajipanga kutojitosheleza
Wenyewe

Yupo Inzi ajulikanaye kama inzi maembe kwa jina la kitaalamu bactrocera invadens husababisha funza ambao huharibu maembe

Funza anayejitokeza baada ya mayai kuanguliwa huishi kwa kula nyama ya maembe na kusababisha vidonda ndani ya embe na matokeo yake ni kuoza kwa embe.

Mara nyingi funza huchangia kwa kiasi kikubwa kushusha thamani ya embe na kufanya soko lake kuanguka

Wadudu wanachangia kuharibu soko la embe kutokana na kufanya embe kuoza mapema kabla ya kuiva na kupelekwa sokoni

Wapo wadudu mbalimbali ambao wanaweza kuharibu maembe kama vile Inzi ambao hutoboa na kutaga mayai ndani ya embe na husababisha embe kudondoka mtini

Tuna wakulima wengi wa maembe sehemu nyingi hapa Tanzania kama Kilimanjaro Tanga na hata Morogoro ambapo mda sio mrefu watakuwa na elimu kuhusu kilimo cha maembe

Ijapokuwa sio wakulima wote wana elimu kuhusu kilimo endelevu cha maembe na magonjwa yanayo athiri zao la maembe lakini elimu hawezi kuwa kuta wote kwa wakati mmoja

Watalaam wa Wizara pamoja na wa Halmashauri huvitembelea vijiji mbalimbali na kukutana na serikali ya kila kijiji husika ili kuwaewesha kazi inayokusudiwa kufanyika katika vijiji vyao.

Katika hatua zote ushirikishwaji wa wakulima unazingatiwa ili kukifanya kilimo hiki kuwa endelevu.Ili kutimiza azma hiyo Wizara imekwisha fanya mabo mengi mfano

Wizara imekiimarisha Bustani ya kuzalisha miti ya matunda ya Mpiji huko Bagamoyo pamoja Pampu za maji 5 ambazo zimenunuliwa.

Matenki ya maji 5, moja la lita 3,000 na manne ya lita 2,000 kila moja yamenunuliwa ili kukizi mahitaji muhimu.

Watanzani tuna takiwa kuiga mfano wa Colombia ambayo huwa inapata dola za marekani mill.200 kwa mwaka kwa kuuza maembe Ulaya pesa ambayo kwa Tanzania ni sawa na mazao mawili

Ili kufikia lengo la kukuza soko la maembe kwa, mkulima anatakiwa kupalilia shamba lake pamoja na kusambaza dawa za mda mfupi

mwisho

mahindi ya kuchoma huleta hasara kubwa zaidi ya faida

mahindi ya kuchoma huleta hasara kubwa zaidi ya faida

Na Bashir Salum

Katikamaisha ya watu wa mjini hasa maeneo ya pwani kama mikoa ya pwani,dare s salaam na hata mkoa wa morogoro kwa wale wasiokuwa wakulima au wale wanaopita mji miji hiyo kama watembeaji huweza kutashangazwa na majira ya mwaka katika maeneo hayo


Wapo watu waishio katika maeneo haya ambao hata kufahamu kuwa vuli au maskaa yanaanza lini au yanakwisha lini kwao ni mtihani kabisa lakini hii inatokna na ukweli kwamaba hata zile dalili za upatikanaji wa vitu fulani kwa kipindi fulani humfanya mtu kutambua misimu ya mwaka

Mfano kule kijijini kwangu huwa hata mtoto wa darasa la tatu anaweza kutofautisha vipindi kutokana na kufahamufika kwamba bidhaa kama mahindi maharage vina msimu wake hivy kuelewa fika misimu hiyo


Katika mikoa tulioitaja utakuta bidhaa ya mahindi ya kuchoma inapatikana katika kipindi chote cha mwaka mzima wakati mikoa kama Dar es salam hakuna wakulima wa mahindi

Ukiangalia kwa sasa biashara ya mahindi ya kuchoma imeenea kila kona huwezi kupiupita mji fulani bila kuwaona wawili watatu waaendesha biashara zao

Mimi binafsi siwachuukii wafanya biashara wa mahindi ya kuchoma ambao kwa hapa mjini utakuta ni wengi sana na wanaendesha maisha yao kutokana na biashara hiyo

Lakini! Tufikirie yahaya mahindi yanatoka wapi! Na yanalimwa na nani? Hivi mkulima wa kawaida anafaidika vilivyo kutokana na bidhaa hii, hapo mi ndio sasa naanza kuingiwa na wasiwasi juu ya hilo

Je ni huyu mkulima anayetumia jembe la mkono au ni yule ana anayetumia teknolojia katika kulima na kupanda halafu anayetengemea mvua ?

Au ni yule mkulima ambaye haitaji mvua anagharamika kutengeneza miundo mbinu ya umwagiliaji na anayetumia teknolojia ambazo kwa kawaida huwa wengi wao huenda wamechukua mkopo!

Mimi nimeshawahi kuishi Morogoro kama miaka mitatu hivi kwa kweli nilikua nikijionea mwenyehe jinsi jinsi magari yanavyoingia mashambani kununua mahindi mabichi

Katika maeneo hayo huwa wakulima hukadiria eneo kwamba kutoka hapa mpaka hapa utanoipa kiasi fulani bila kujali kuwa makadirio ya namna ile yeye anaweza kupunjwa na kazi aliofanya ni kubwa zaidi

Kumbumka mchoma mahindi unaemuona hapa mjini nakuuzia muhindi shilingi 250 na 300 na hata wengine huuza kwa 400 kwa muhindi moja

Ukifika katika masoko ya mahindi pale tandika au tandale utakuta muhindi mmoja huuzwaa kati ya shilingi 120 mpaka 170 au kwa wengine 200 pia huuza

Maswali mengi tunajiuliza huku tukiona kama mkulima atakuwa na hali ngumu kama sokoni hiyo ndio bei yeye atakuwa kauza kwa shilingi ngapi kwa kila hindi moja ?

Inawezekanna wewe ukawa shahidi namba mbili hata kwa kujionea jinsi magari yanavyomwagika kutoka mikoani yakiwa yamesheni mahindi mabichi kama hujaona tembelea masoko ya tandika au tandale ili uweze kuwa shahidi mzuri

Huko vijijini mi sijawahi kuona au kusikia soko kama haya ya hapa dar ambapo yanauzwa mahindi mabichi na bei zinazojulikana ,kama nikweli hakuna ni wazi kuwa mkulima mdogo anapunjwa na anahitaji ushauri nasaha

Wakati fulani wizara ya kilimo chakula na ushirika ilikaza uuzwaji wa mazo ya kiwa shambani kwa kuwa walilitambua hili na dawa ya kumsaidia mkulima ilikuwa ni kukazata ununuzi wa mazao yakiwa shambani

Mkulima atakapopewa labda laki mbili au tatu akauza mahindi yote alioko shambani huenda anaona zile ni pesa nyingi sana kwa kuwa zimekuja kwa pamoja na huenda labda kwa wakati ule alikuwa na shida

Lakini ukweli ni kwamba kama yale mahindi angeyavuna naamini angeweza kupata faida zaidi kuliko alichokifanya kwa muda ule

Kwani hata ukipiga mahesabu, gharama za kulima ,za kupand , kuhudumia mmea mpaka ukazaa na mpaka mteja akaupenda kuunuua kwa kiasi hicho utagundua kuwa gharama aliingia sio sawa na gharama aliouzia

Na hili ndio maana kila siku mkulima njaa kwake haishina kila siku serikali inawapa msaada , na sio kweli kuwa wanakosa kabisa ijapokuwa pia sio wote wanapata

Kama mkulima anaweza kupewa labda laki tatu au nne hawezi kuzitumia kwa muda wa miezi sita lakini kama hayo mahindi angeyavuna kwa utaratibu na kuyahifadhi vizuri angayeweza kuyauza kwa bei nzuri na kwa kipimo kinachoeleweka